Hili Balaaa!!! Baada ya Shiole na Nuh Mziwanda Kukutanishwa, Je Kuna Uwezekano Wakarudiana?

Ijumaa iliyopita kupitia kipindi cha WikiendChartShow cha Clouds Tv 
kiliwakutanisha Nuh Mziwanda na Shishi ambao wameachana,Je? Kuna 
uwezekano wapenzi hao wakarudiana?
’Nimeficha mambo yake mengi sana kwa maslahi ya penzi letu,yeye anajua 
mambo gani aliyokuwa akinifanyia ambayo alikuwa hastahili kunifanyia 
kama mpenzi wake,alikuwa akinichukulia poa tu,nilikuwa nikionekana 
mwanaume mbele za watu lakini haikuwa kweli,nilikuwa naumia ndani kwa 
ndani bila watu kujua,nimemsamehe sina tatizo nae,’’Nuh.
‘’Nuh na Shishi ni marafiki zangu nawajua vizuri walipokuwa wakigombana 
nilikuwa niwasuruhisha yanaisha sasa kipindi hiki walivyogombana 
sikuwepo nilikuwa Kigoma,ningekuwepo yasingefikia haya ila ninachojua 
hawa wanapenda cha msingi mmoja wao ajishushe,’’Baba Levo.
‘’Unajua ukiongea na Nuh ukimuuliza unampenda Shilole hana jibu kamili 
lakini ninavyoona wanapenda na watarudiana tu,ila Nuh anawahofia ndugu 
zake ambao hawamtaki Shishi na mambo mabaya ambayo aliyokuwa 
akimfanyia,’’ Soudy Brown.

0 comments: