Safi:Serikali ya ahidi kuendelea kutatua kero za wasanii

Waziri wa Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (aliyevaa batiki) na Waziri wa 
Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Mhe. Charles Mwijage wakiwa katika picha
 ya pamoja na baadhi ya wasanii mara baada ya kumaliza kikao na Kamati 
ya wasanii leo jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Frank Shija-WHUSM
Waziri wa Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (mwenye shati la batiki) 
akizungumza na wajumbe wa Kamati ya wasanii wa Muziki inayofuatilia 
suala la malipo ya mrabaha kutokana na kazi zao Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Viwanda, Biashara na 
Uwezeshaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza na wajumbe wa Kamati ya 
wasanii wa Muziki inayofuatilia suala la malipo ya mrabaha kutoka kwa 
vyombo vya habari na miito ya simu. Kushoto ni Waziri wa Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye na kulia ni Katibu 
Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mungereza leo 
jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya 
ambaye pia ni Kiongozi wa Kamati ya wasanii wa muziki Bw. Nickson Simon 
kwa jina la kisanii Nikki wa Pili akiwasilisha hoja za kwa niaba ya 
wasanii wenzake wakati wa kikao baina yao na waheshimiwa Mawaziri wa 
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja Mhe. Nape Moses Nnauye na 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Mhe. Charles Mwijage leo 
jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sana Bibi. 
Leah Kihimbi na kushoto ni msaanii Ditto.
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya 
ambaye pia mjumbe wa Kamati ya wasanii wa muziki akichangia mada wakati 
wa kikao baina yao na waheshimiwa Mawaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa 
na Michezo pamoja Mhe. Nape Moses Nnauye na Waziri wa Viwanda, Biashara 
na Uwezeshaji Mhe. Charles Mwijage leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na msanii mkongwe wa
 muziki wa injili Bw. Cosmas Chidumule mara baada ya kumaliza kikao na 
Kamati ya wasanii leo jijini Dar es Salaam.
0 comments: