Wajane Wawili Wauawa Kwa Kukatwa Mapanga Wakidaiwa Kusambaza Kipindupindu Mkoani Mbeya

Wajane
 wawili wa Kitongoji cha Bulinda wilayani Kyela wameuawa kwa mapanga 
wakidaiwa kusambaza ugonjwa wa kipindupindu baada ya kufiwa na waume zao
 katika eneo hilo.
Waliouawa ni Geneli Kapwela (65) na Rahabu Bungulu (70) waliokuwa wakiishi peke yao.
Kamanda
 wa Polisi  Mkoa wa Mbeya  Ahmed  Msangi  alisema  jana kuwa  wajane  
hao  waliuawa  juzi  baada  ya  kipindupindu  kuhusishwa  na  imani za 
kishirikina.
Takwimu  za  mauaji toka polisi zinaonyesha  karibu watu wawili wanauawa  mkoani  Mbeya  kwa  imani  za  kishirikina

0 comments: