EWURA katika ubora wake : Yasema Nchi Inaakiba Ya Kutosha Ya Mafuta

SERIKALI
 imewatoa hofu Watanzania kuhusu uwepo wa mafuta ya kutosha nchini baada
 ya kuamriwa kurudishwa kwa meli iliyokuwa imebeba shehena ya mafuta 
yenye kiwango kisichofaa.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa 
Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (Ewura), Felix 
Ngamlagosi, alisema kuna akiba ya kutosha na hivyo watanzania wasiwe na 
hofu kwani kurudishwa kwa meli hiyo hakuna athari zozote kwa upande wa 
mafuta.
Alisema
 ipo akiba ya mafuta ya kutosha na kwamba Ewaura inaendelea kupokea 
shehena za mafuta kama kawaida na kwa kiasi kitakachoendelea kutosheleza
 mahitaji ya nchi. 
Aliongeza
 kuwa hadi kufikia Januari 8 mwaka huu kulikuwa na kiasi cha lita 
255,052,370 kwa ajili ya soko la ndani, lita milioni 143.547 kwa ajili 
ya soko la nje, na lita milioni 27.875 za dizeli kwa ajili ya matumizi 
ya migodi.
“Wananchi
 wasiwe na hofu. Kilichofanywa na TBS hakijaathiri chochote. Kwa takwimu
 hizi ni dhahiri kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta na bado 
tunaendelea kupokea,” alisema Ngamlagosi.
Aidha
 alisema katika kipindi cha Desemba 2015 na Januari 2016 bei za mafuta 
katika soko la dunia zimeendelea kushuka na kwamba bei za mafuta katika 
soko la Tanzania zilifuata mwenendo wa bei za mafuta katika soko la 
dunia.
Katika
 kudhibiti ubora wa mafuta, alisema Ewura inaendelea kuchukua sampuli 
kwenye vituo vya mafuta, maghala makubwa ya kuhifadhi mafuta na magari 
ya kubeba mafuta, lengo likiwa ni kukagua ubora wa mafuta.

0 comments: