News: Utambulisho Wa Mwanamuziki Mpya Wa Studio Ya Muziki Ya “the Industry”

Uongozi
 wa Studio ya Muziki ya The Industry iliyoko chini ya Wanamuziki 
Producer Nahreel na Aika Marealle unapenda kuchukua Nafasi hii 
kuwatangazia Umma Kuwa kuanzia Tarehe 14 January 2016 Wamemuingiza 
Msanii mpya wa Kike aitwaye Rosa Ree, Rose Ree ni muimbaji wa Muziki 
aina ya Rap ambae kazi zake zitaanza kusikika/Kuonekana siku si nyingi 
kuanzia sasa katika Redio Mbali mbali na TV Stations za Tanzania na nje 
ya nchi.
Kama
 wasikilizaji na watazamani tunaomba Kumuunga mkono Msanii huyu mpya 
Kwani tuna uhakika hatawaangusha katika kuwaletea burudani Katika 
Masikio na macho yenu pindi kazi zake zitakapoanza kutolewa hivi 
karibuni.
The
 Industry ni studio na kampuni ya muziki ambayo ipo chini ya kundi la 
music lenye Mafanikio makubwa la Navy Kenzo ikisimamiwa na Producer 
Nahreel na msaidizi wake Aika Marealle
Wasanii
 Baadhi Waliokwisha fanya kazi na Studio ya The Industry mpaka sasa toka
 kuanzishwa kwake hivi karibuni ni Diamond Platnumz na wimbo wake wa 
Nana, Nikki wa Pili na wimbo wa Baba Swalehe, Joh Makini na nyimbo zake 
kama Don’t Bother na nusu nusu.
Imetolewa na,
The Industry PR
John Kiandika

0 comments: